Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 12:06

Serikali na upinzani Kongo wakaribia kufikia makubaliano


Askofu Marcel Utembi, mpatanishi wa Kanisa la kikatoliki awasili kwenye majadiliano mjini Kinshasa, Disemba 21 2016
Askofu Marcel Utembi, mpatanishi wa Kanisa la kikatoliki awasili kwenye majadiliano mjini Kinshasa, Disemba 21 2016

Majadiliano kati ya serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na upinzani kupitia upatanishi wa viongozi wa Kanisa Katoliki, yaliendelea hadi Ijuma usiku bila ya kupatikana ufumbuzi wa mwisho wa mzozo wa kisiasa nchini humo.

Mzozo huo umezushwa na kukata kwa Rais Joseph Kabila kuondoka madarakani mhula wake ulipomalizika tarehe 19 Disemba 2016, na kukupelekea ghasia kati ya wananchi na vikosi vya usalama katika miji mikuu kwa siku tatu.

Wakazi wa Kinshasa wakiimba nyimbo za kumtaka Kabila aondoke madarakani
Wakazi wa Kinshasa wakiimba nyimbo za kumtaka Kabila aondoke madarakani

Matumaini ya kufikiwa makubaliano yalijitokeza Alhamisi pale upinzani na serikali kukubali kwamba Rais Kabila ataendelea kubaki madarakani hadi kuitishwa uchaguzi hapo disemba 2017.

Viongozi wa pande zote walikubalkiana kwamba Kabila hatoweza kugombania tena uchaguzi na hakuna mabadiliko ya katiba yatafanyika mnamo kipindi cha mpito cha mwaka mmoja.

Kizingiti kikubwa siku ya ijuma kufuatana na mwandishi wa Sauti ya amerika mjini Kinshasa Saleh Mwanamilongo ni kuhusu kuundwa tume ya kufuatilia utekelezaji wa makubaliano. Upinzani wanataka paundwe baraza la kufuatilia mpito kuliko tume na liongozwe na Etienne Tshisekedi, lakini serikali inakubali kuwepo na tume pekee iisiyo na mamlaka makubwa.

Muandamanaji akikamatwa na polisi wa kikosi maalum cha kupambana na ghasia.
Muandamanaji akikamatwa na polisi wa kikosi maalum cha kupambana na ghasia.

Hali ingali tete huko Kongo ambako kuna baadhi ya wananchi waloeleza kuridhika kwao na Kabila kubaki hadi mwakani lakini kutogombania tena uchaguzi,huku wakazi wa mashariki wakisema makubaliano hayo ni ukiukaji wa katiba.

XS
SM
MD
LG