Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 20, 2024 Local time: 04:42

Saudia yakaribisha kwa tahadhari mkataba wa nuklia wa Iran


Wajumbe wa mazungumzo ya mkataba wa nuklia wa Iran
Wajumbe wa mazungumzo ya mkataba wa nuklia wa Iran
Saudi Arabia imeungana na nchi nyingine za ghuba ya kiarabu kukaribisha kwa tahadhari makubaliano ya nuklia na Iran yaliyofikiwa na nchi zinazopingana na Iran na kundi la nchi zenye nguvu dunaini.

Katika taarifa iliyotolewa Jumatatu serikali ya Saudi Arabia ilisema makubaliano hayo yanaweza kuwa hatua ya mwanzo ya kupata suluhu kuhusu mzozo wa nuklia wa Iran na kwa malengo mazuri.

Chini ya makubaliano yaliyotiwa saini mjini Geneva Iran ilikubali kutoendelea na sehemu ya programu zake za kwa miezi sita, nayo iondolewe vikwazo vya kiuchumi kwa miezi sita na nchi zenye nguvu duniani.
XS
SM
MD
LG