Katika uchaguzi uliofanyika jana Ijumaa, Hassan Rouhani alimshinda mpinzani wake wa karibu Ebrahim Raisi aliyepata asilimia 39.8.
Ebrahim Raisi anayeungwa mkono na Kiongozi wa Kidini wa nchi hiyo Ayatollah Ali Khamenei, ni mmoja wa viongozi wa kidini mwenye msimamo mkali dhidi ya sera za mataifa ya magharibi.
Uchaguzi huo ulikuwa jaribio kubwa kwa Rais Rouhani kufuatia sera zake za mageuzi ambapo ameifanya Iran kuwa karibu na mataifa ya magharibi, na kuweza kuingia mkataba na mataifa yenye nguvu juu ya mradi wake wa nyuklia.