Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 25, 2024 Local time: 11:48

Rais Magufuli atangaza baraza la mawaziri Tanzania


Rais wa Tanzania, John Magufuli
Rais wa Tanzania, John Magufuli

Rais wa Tanzania John Magufuli ametangaza baraza lake jipya la mawaziri wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lenye wizara 18 lakini litakuwa na mawaziri 19.

Ripoti ya Dina Chahali kutoka Dar Es Salaam.

please wait

No media source currently available

0:00 0:02:38 0:00
Kiungo cha moja kwa moja

Katika mtiririko huo kuna baadhi ya wizara zitakuwa na waziri pekee bila ya kuwa na naibu waziri ambapo lengo kuu ni kutimiza ahadi ya kuwa na baraza dogo lenye kasi ya ufanyaji kazi na kupunguza gharama za matumizi ya serikali yasiyo ya lazima.

Rais magufuli alisema baraza lake la mawaziri halitakuwa na semina elekezi na fedha zilizotengwa shilingi bilioni mbili kwa shughuli hiyo zitaelekezwa katika ufanyaji kazi mwingine wa kuboresha maendeleo ya wananchi kama vile madawati au kwenye utoaji wa elimu bure.

XS
SM
MD
LG