Rais wa Marekani Barack Obama amemsihi rais wa Gabon Ali Ben Bongo kuondoa rushwa na kulinda haki za binadamu katika nchi ya Afrika magharibi.
Bw. Obama alikutana na Bw.Bongo huko White house alhamisi licha ya maswali kuhusu tuhuma za rushwa katika familia ya Bongo na serikali.
White house inasema Bw.Obama amefurahishwa na mageuzi ambayo Gabon imechukua chini ya Bw. Bongo kuweka uwazi zaidi na uwajibikaji wa serikali.
Gabon inashikilia urais wa kuzunguka wa baraza la usalama la Umoja wa mataifa.