Pakistan imelaumu Marekani kwa kusambaratisha juhudi za Islamabad za kufadhili mashauriano ya kumaliza mzozo ulioko Afghanistan, ikisema kuwa kiongozi alieuwawa wa kundi la Taliban hakua anazuia mazungumzo hayo.
Waziri wa Sera za Kigeni wa Pakistan, Sarjat Aziz, ameambia wanahabari mjini Islamabad mapema leo kuwa maafisa wa Pakistan waliodai kuwasiliana na Taliban wamesema kuwa kiongozi huyo alieuwawa Mullah Mansoor alikuwa anajitayarisha kuja kwenye meza ya mazungumzo.
Mansoor alikuwa akisafiria kwenye gari akitoka Iran kupitia kusini magharibi mwa Pakistan katika jimbo la Baluchistan Jumamosi wakati silaha kutoka kwa Marekani ilipomuuwa pamoja na dereva wake.