Serikali ya Niger inasema wanajeshi 46 na raia 28 waliuwawa mwishoni mwa juma wakati vikosi vikipambana na wanamgambo wa Boko Haram kudhibiti kisiwa kimoja katika ziwa Chad.
Maafisa wanasema kwamba wanamgambo156 pia waliuwawa katika mapambano ambayo yalianza baada ya Boko Haram, kushambulia kisiwa cha Karamga siku ya Jumamosi.
Jeshi la Niger linasema toka kipindi hicho wamefanikiwa kushikilia kisiwa hicho.
Niger, pamoja na Nigeria, Chad na Cameroon, siku za karibuni zimemekuwa zikifanya mashambulizi kumaliza kadhia inayofanywa na Boko Haram.
Mpaka sasa Boko Haram, imesha gharimu maisha ya watu 10,000 na kuwakosesha makazi zaidi ya watu milioni moja kaskazini mashariki mwa Nigeria.