Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir amesema ana uhakika serikali yake na serikali ya Sudan watahusuluhisha mzozo wao juu ya eneo lenye utajiri wa mafuta la Abyei.
Katika mahojiano jumapili na VOA Bw. Kiir alisisitiza kuwa sheria ya kimataifa inaunga mkono eneo hilo kuwa sehemu ya Sudan Kusini . Amesema Kaskazini wangeshajiondoa kwenye eneo hilo siku nyingi kama lingekuwa halina mafuta.
Bw. Kiir rais wa nchi mpya duniani aliongea na VOA huko New York baada ya kwenda huko kwa mara ya kwanza kama kiongozi wa nchi katika mkutano wa baraza kuu la umoja wa mataifa.