Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 12:33

Mzozo wa eneo la Abyei utasuluhishwa asema Salva Kiir.


Rais Barack Obama alipokutana na rais wa Sudan Kusini Salva Kiir .
Rais Barack Obama alipokutana na rais wa Sudan Kusini Salva Kiir .

Rais Salva Kiir asema kuwa sheria ya kimataifa yaunga mkono eneo la Abyei kuwa la Kusini.

Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir amesema ana uhakika serikali yake na serikali ya Sudan watahusuluhisha mzozo wao juu ya eneo lenye utajiri wa mafuta la Abyei.

Katika mahojiano jumapili na VOA Bw. Kiir alisisitiza kuwa sheria ya kimataifa inaunga mkono eneo hilo kuwa sehemu ya Sudan Kusini . Amesema Kaskazini wangeshajiondoa kwenye eneo hilo siku nyingi kama lingekuwa halina mafuta.

Bw. Kiir rais wa nchi mpya duniani aliongea na VOA huko New York baada ya kwenda huko kwa mara ya kwanza kama kiongozi wa nchi katika mkutano wa baraza kuu la umoja wa mataifa.

XS
SM
MD
LG