Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 12:04

MERRY KRISMAS


Baba Mtakatifu Benedict akisalia misa ya mkesha wa Kristmas katika kanisa la St. Peter's Basilica Vatican Dec. 24, 2012
Baba Mtakatifu Benedict akisalia misa ya mkesha wa Kristmas katika kanisa la St. Peter's Basilica Vatican Dec. 24, 2012
Baba Mtakatifu Benedict ameombea amani, hasa Mashariki ya Kati, katika misa yake ya mkesha wa Krismas, wakati wakristo kote duniani wanajiandaa kusherehekea leo kuzaliwa kwa Yesu Kristo zaidi ya miaka 2,000 iliyopita.

Akihutubia waumini katika kanisa la Mtakatifu Petro Jumatatu jioni, kiongozi huyo wa kanisa katoliki alitoa wito wa kumaliza umwagaji damu Syria, Lebanon, Iraq na nchi za jirani. Aliombea pia watu wa Israel na Palestina kuishi pamoja kwa amani.

Maelfu wa watalii kutoka kote duniani walikusanyika katika mji wa Bethlehem, Ng'ambo ya Magharibi kusherehekea sikukuu hiyo mahali ambapo Wakristo wanaamini Yesu Kristo alizaliwa.

Jumanne maelfu ya Wakristo kote duniani watamiminika katika makanisa kuhudhuria misa ya krismas na kufuatiwa na sherehe ikiwa ni chakula, vinywaji na kutembeleana. Katika nchi za Afrika Mashariki na Kati wakristo wengi wanatazamiwa kusherehekea kwa mikusanyiko ya kila namna kuanzia starehe hadi ibada.

Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Amerika inawatakiwa wasikilizaji wetu wote Krismas Njema
XS
SM
MD
LG