Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 18:26

Mazungumzo ya DRC kuanza Ijumaa Kampala


Wapiganaji wa M23 wakiondoka karibu na mji wa Sake kiasi cha kilomita 42 magharibi mwa Goma Novemba 30,2012
Wapiganaji wa M23 wakiondoka karibu na mji wa Sake kiasi cha kilomita 42 magharibi mwa Goma Novemba 30,2012
Waasi huko Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo-DRC, Ijumaa watafanya mazungumzo na serikali ya Congo.

Msemaji wa serikali ya Uganda Fred Opolot anasema wajumbe kutoka serikali ya Congo na kundi la waasi la M23 wataanza vikao vya awali mjini Kampala vitakavyolenga namna ya kutatua mgogoro wao.

Anasema mazungumzo yatalenga juu ya kanuni za msingi kwa mikutano ya baadae na miongozo kwa waangalizi ambao watafuatilia maeneo ya mzozo huko mashariki mwa DRC.

Kundi la m23 liliondoka kutoka mji wa Goma uliopo mashariki mwa DRC wiki iliyopita lakini kundi hilo linatishia kuuteka tena mji huo kama serikali inashindwa kuanza mashauriano.
Waasi walilishinda jeshi la Congo katika mifululizo kadhaa ya mapigano mwaka huu.

Jopo moja la wataalamu wa Umoja wa Mataifa linaishutumu Uganda na Rwanda kwa kulisaidia kundi la waasi kitu ambacho nchi zote zinakanusha.

Taarifa ya Alhamis kutoka kwa Opolot ilisema “Uganda kama mwenyekiti wa sasa wa mkutano wa kimataifa wa eneo la maziwa makuu inaendelea kuratibu utaratibu wa amani huko DRC”.

Kundi la M23 limeundwa na waasi wa zamani ambao waliingizwa katika jeshi la Congo kufuatia mkataba wa amani wa mwaka 2009. Waasi walijitoa kwenye jeshi mapema mwaka huu wakidai kubaguliwa na kupatiwa huduma mbaya.

Mapigano yamewakosesha makazi zaidi ya watu 100,000 katika jimbo la Kivu kaskazini huko Congo na kusababisha kuwepo hali mbaya ya kibinadamu katika eneo hilo.
XS
SM
MD
LG