Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 17:56

Mashirika ya kiraia Beni yawataka raia wasilipe kodi kwa serikali ya DRC


Eneo la Beni, Kivu kaskazini huko Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo-DRC
Eneo la Beni, Kivu kaskazini huko Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo-DRC

Mashirika ya kiraia huko Beni, Lubero na Butembo katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo-DRC yamewataka wananchi wasilipe kodi yoyote ya serikali hadi kiongozi wa jeshi la Congo FARDRC atakapo tembelea eneo la Beni na kujionea mwenyewe hali ya kiusalama ilivyo na kusitisha mauwaji ya watu kote eneo la Beni na Lubero.

please wait

No media source currently available

0:00 0:02:58 0:00
Kiungo cha moja kwa moja

Akizungumza kwa niaba ya mashirika hayo baada ya mkutano uliofanyika katika mji wa Butembo ambapo mashirika yalikutana kufuatia mgomo wa siku tatu, bwana Kizito Binhangi alisema “ndio tunakuhakikishia tulimwandikia rais barua baada ya kuona kwamba mauaji yameendelea kwenye eneo hilo na ndio maana waliwataka wakazi wasilipe kodi yeyote kwa ni hawawezi kufanya hivyo huku wanashikiliwa”.
Hatua hiyo ilichukuliwa katika kikao huko Butembo ambako
mashirika yote yalikutana baada ya kufanyika mgomo huo mwishoni mwa wiki.

XS
SM
MD
LG