Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 22:50

Mashauriano ya amani Sudan yaleta imani


Makundi ya upinzani pamoja na vikosi vyenye silaha vimeelezea imani yao wakati wa mkutano wa amani kati ya wajumbe kutoka Quatar na vingozi wawili, Mini Arku Minawi na Jibreel Ibrahim.

Vingozi hao wawili wanasemekana kuwa na wasi wasi kuhusu mashauriano hayo.

Msemaji wa harakati ya Freewill, Mohamed Abdullah Wadabouk, amesema mashauriano hayo yanatarajiwa kubadilisha hali ya kisiasa miongoni mwa vikundi tofauti vilivyoko nchini Sudan na pia mataifa ya kigeni.

Nashar Osman Nahar, ambae ni katibu wa kisiasa kwenye vuguvugu la haji na usawa, amesema kuwa mashauriano hayo kati ya vikundi vya Dafur na Quatar ni hatua mwafaka ya kupatikana kwa amani kwenye eneo la Darfur.

XS
SM
MD
LG