Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 25, 2024 Local time: 07:04

Marekani yaishutumu Syria kushambulia magari ya misaada


watoto wakiwa wanatembea karibu na jengo lililoharibiwa
watoto wakiwa wanatembea karibu na jengo lililoharibiwa

Malori hayo yalilengwa na ndege za wanamgambo, kwa mujibu wa shirika linalofuatilia haki za binadamu nchini Syria, la Syrian Observatory for Human Rights.

Marekani inaishutumu Syria kwa kufanya mashambulizi ya anga kwenye malori ya kutoa msaada wa kibinadamu Jumatatu ambayo yalijaribu kulifikia eneo la Aleppo.

Umoja wa Mataifa na chama cha hilali nyekundu cha Syria wamesema taasisi za makundi mbali mbali zinasafirisha msaada wa chakula kutoka Uturuki kwa ajili ya maelfu ya watu waliokumbwa na vita.

Hakuna taarifa zaidi iliyotolewa. Malori hayo yalilengwa na ndege za wanamgambo, kwa mujibu wa shirika linalofuatilia haki za binadamu nchini Syria, la Syrian Observatory for Human Rights.

Shambulizi limekuja wakati wa makubaliano ya wiki moja ya kusitisha mapigano ambayo hayakufuatwa, huku jeshi la Syria likilaumu kuvunjika kwa makubaliano hayo kufuatia vikosi vya upinzani vinavyoungwa mkono na Marekani.

XS
SM
MD
LG