Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 08:26

Marekani kusikiliza ushahidi wa Uturuki


Makamu wa Rais wa Marekani, Joe Biden anasema “White House” inadhamiria kusikiliza kila ushahidi utakaowasilishwa na Uturuki kabla ya kuamua kumrudisha kiongozi wa dini ya Kislamu, Fethullah Gulen.

Kiongozi huyo anaishi katika jimbo la mashariki la Pennsylvania na Uturuki inataka kurudishwa mchini kwa kiongozi huyo haraka kwa shutuma za kupanga jaribio la mapinduzi mashitaka ambayo yamekanwa.

Bwana Biden alikutana mjini Ankara hapo jana na Rais wa wa Uturuki, Recep Tayyip Erdonag.

Alijitahidi kutaka subira kutoka kwa rais Erdogan kwa kumueleza kwamba mahakama za Marekani zinataka ushahidi wa kutosha kabla mtuhumiwa hajakabidhiwa kwa nchi nyingine.

XS
SM
MD
LG