Korea Kusini imesema itarudia tena matangazo ya propaganda kutumia kipaza sauti ndani ya Korea kaskazini Ijumaa ikiwa ni majibu yao kutokana na majaribio ya nyuklia ya Pyongyang mapema wiki hii.
Hatua hiyo ya Seoul inakuja wakati rais Barack Obama ameahidi kufanya kazi na viongozi wa Korea kusini na Japan katika kuwasilisha jibu la pamoja kwa Korea Kaskazini kwa kile wanachodai ilikuwa bomu la Hydrogen.
Waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe ameongea na wabunge juu ya Korea Kaskazini.