Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 21:12

Wanamgambo wawachinja polisi 40 DRC


Polisi wa kupambana na ghasia wa DRC wakiondowa vizuizi vya barabarani Kinshasa December 10, 2011.
Polisi wa kupambana na ghasia wa DRC wakiondowa vizuizi vya barabarani Kinshasa December 10, 2011.

Karibu maafisa 40 wa polisi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wameuliwa kwa kukatwa mapanga na wanamgambo wa kundi la Kamwina Nsapu katika jimbo la kati la Kasai.

Kwa mujibu wa rais wa bunge la Kasai Francois Kalamba, wanamgambo hao walishambulia msafara wa magari ya polisi uliokuwa unasafiri kutoka mji wa Tshikapa kuelekea mji mkuu wa jimbo la Kasai wa Kananga waliposhambuliwa Ijumaa na wanamgambo hao.

Kalamba amesema walioshuhudia wameeleza kuwa wanamgambo waliwaachilia huru maafisa sita kwa vile walikuwa wanazungumza lugha ya Tshiluba inayotumika eneo hilo.

Anasema wanamgambo hao ambao kawaida huwa na mapanga, waliiba bunduki na silaha za polisi na kukimbia pamoja na magari yao.

Uasi katika eneo la kati ya DRC ulianza mwezi Agosti mwaka jana na umeenea katika majimbo kadhaa ya eneo hilo.

Hata hivyo siku ya Jumamosi wizara ya mambo ya ndani ya serikali kuu imetangaza kwamba kuna wanamgambo 400 wamejisalimisha wiki hii katika jimbo hilo la Kasai.

XS
SM
MD
LG