Mamilioni ya Wamisri walijipanga kwenye mistari mirefu jumatano kupiga kura katika uchaguzi wa kwanza wa rais tangu rais Hosni Mubarak kujiuzulu mwaka jana kati kati ya upinzani mkubwa.
Maandalizi ya uchaguzi huo wenye mvutano mkali kwa kiasi kikubwa unawahusisha wagombea unawahusisha wale ambao wana uhusiano na bwana Mubarak dhidi ya Waislam wanaojaribu kuunda ushirikiano mpya. Kwa jumla wagombea 13 wako kwenye karatasi ya kura lakini mmoja amejitoa kwenye kinyang’anyiro . Uchaguzi utakuwa wa siku mbili.
Mwandishi wa Sauti ya Amerika Elizabeth Arrot alikuta makundi makubwa ya watu kwenye vituo vya kupigia kura vya Cairo.
Kiasi cha Wamisri milioni 50 wanastahili kupiga kura . Miongoni mwao ni Gihad Amr ambaye anasema hajui atarajie nini.
Huku maandamano makubwa yakiendelea wiki kadhaa kabla ya uchaguzi kumekuwa na wasi wasi kuhusu ghasia.
Mashirika ya habari yanasema Polisi mmoja alipigwa risasi na kuuwawa nje ya kituo cha kupigia kura mjini Cairo kwenye mapigano kati ya wafuasi wa wagombea wawili wa nafasi ya urais.