Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 18, 2024 Local time: 10:13

Waasi wa Mali watakiwa kukata uhusiano na magaidi


A magnetic filament of solar material erupted on the sun in late September, breaking the quiet conditions in a spectacular fashion. The 200,000 mile-long filament ripped through the sun's atmosphere, the corona, leaving behind what looks like a canyon of of fire. (NASA/Solar Dynamics Observatory)
A magnetic filament of solar material erupted on the sun in late September, breaking the quiet conditions in a spectacular fashion. The 200,000 mile-long filament ripped through the sun's atmosphere, the corona, leaving behind what looks like a canyon of of fire. (NASA/Solar Dynamics Observatory)
Mpatanishi wa Afrika Magharibi amewaambia waasi kaskazini mwa Mali lazima wajitenge na magaidi kabla ya mazungumzo ya amani kuanza.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Burkina Faso, Djibril Bassole, ambaye anaiwakilisha Jumuiya ya uchumi ya mataifa ya Afrika Maghairbi - Ecowas, alitembelea eneo la kaskazini mwa Mali na kukutana na viongozi wa kundi la wanamgambo wa kiislamu la Ansar Dine katika mji wa Kidal.

Akiongea na waandishi wa habari katika mji mkuu wa Burkina Faso baada ya safari yake, Bassole amesema amewaeleza waasi juu ya matakwa ya Ecowas.

Amesema pia aliutembelea mji wa Gao, ambao unadhibitiwa na kundi jingine la wanamgambo la MUJAO. Alizungumza na viongozi wa eneo hilo lakini si wa kundi la MUJAO.

Ecowas inaongoza juhudi za kieneo kusuluhisha mzozo wa kisiasa wa Mali, ambao ulianza pale wanajeshi walipoiangusha serikali mwezi Machi, na kuwaruhusu waasi kulikamata eneo la kaskazini mwa nchi.
XS
SM
MD
LG