Majaji katika idara ya mahakama nchini Kenya wanalalamikia kuingiliwa kati kwa shughuli zao na maafisa wa serikali kuu huku wakitoa maagizo ya jinsi kesi zinahitaji kuamuriwa.
Aidha wanadai kuwa idara mbali mbali za serikali zinakaidi amri za mahakama na hivyo kuendeleza ukiukaji wa sheria swala aambalo wanadai linapunguza imani ya wakenya katika idara ya mahakama. Sikiliza ripoti yake Liberty Adede akiwa mombasa, Kenya.