Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 13:11

Maharamia wa somalia waachilia raia 22 wa Tunisia waliowateka


Maharamia wa somalia waachilia raia 22 wa Tunisia waliowateka
Maharamia wa somalia waachilia raia 22 wa Tunisia waliowateka

Maharamia wa somalia wameachilia meli iliyokuwa imebeba kemikali na wafanyakazi wote wa tunisia

Maharamia wa Somalia wameachilia meli iliyokuwa imebeba kemikali na karibu wafanyakazi wote wa Tunisia.

Maafisa wa Tunisia wanasema maharamia waliachilia meli ya Hannibal 11, na wafanyakazi wake baada ya kupata malipo ya fidia ya dola milioni 2.

Maafisa wanasema raia 22 wa Tunisia na wafanyakazi wengine tisa waliokuwemo katika meli wako katika hali nzuri na kwamba meli hiyo inaelekea Djibouti.

Meli hiyo ilitekwa novemba mwaka jana ikiwa imebeba mafuta ya kupika kutoka Malaysia kwenda misri.

Wakati huo huo jeshi la umoja wa ulaya linalopambana na maharamia linasema maharamia wameteka meli nyingine ya Indonesia na kuitumia katika jaribio lililoshindwa kuvamia meli nyingine

XS
SM
MD
LG