Marais wa nchi sita zinazounga jumuiya ya Afrika Mashariki wamekubaliana kuanzisha taasisi ya kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili itakayokuwa na makao yake katika visiwa vya Zanzibar.
hatua ya kuanzisha taasisi hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa mapendekezo yaliyotolewa na baraza la mawaziri wa nchi hizo kwenye kikao cha 17 cha marais wa nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki lengo likiwa kukifanya kiswahili kuwa lugha ya ukanda huo.
nchi zinazotarajiwa kutumia lugha ya kiswahili ni pamoja na Kenya, Rwanda, Burundi, Tanzania na Uganda.