Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 15:03

Kesi ya Ruto kuanza jumanne ICC


William Ruto akiwa kwenye chumba cha mahakama ya ICC huko The Hague, Uholanzi, May 14, 2013.
William Ruto akiwa kwenye chumba cha mahakama ya ICC huko The Hague, Uholanzi, May 14, 2013.
Kesi ya naibu rais wa Kenya, William Ruto itaanza Jumanne huko The Hague, Uholanzi kwa shutuma za uhalifu dhidi ya binadamu. Bwana Ruto aliondoka Nairobi Jumatatu kuelekea mahakama ya kimataifa ya uhalifu-ICC akisindikizwa na wafuasi kadhaa.

please wait

No media source currently available

0:00 0:03:06 0:00
Kiungo cha moja kwa moja

Naibu rais anashutumiwa kwa kusaidia kupanga ghasia za baada ya uchaguzi mkuu mwaka 2007 ghasia ambazo ziliendelea hadi mwaka 2008 ambazo ziliuwa zaidi ya watu 1,000 na kuwakosesha makazi zaidi ya watu nusu milioni kutoka kwenye nyumba zao.

Bwana Ruto anashtakiwa pamoja na mtangazaji wa kituo kimoja cha radio mjini Nairobi, Joshua Arap Sang. Wote wanatarajiwa kukana makosa ya mashtaka.
XS
SM
MD
LG