Serikali ya Kenya iliongeza kasi Jumanne katika shughuli za uokozi wa raia wake waliokwama Sudan Kusini baada ya machafuko yaliyozuka baina ya wanajeshi watiifu wa Rais wa nchi hiyo Salva Kiir na walinzi wa naibu wake wa Kwanza Riek Machar wiki moja iliyopita.
Siku ya Jumanne Wakenya zaidi ya 100 walitua uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta huku wakisimulia masaibu yaliyowakumba mjini Juba. Mwandishi wetu wa Nairobi Kennedy Wandera ametuandalia taarifa ifuatayo.