Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 08:26

Vyama vya muungano wa Jubilee Kenya vya vunjwa


Rais wa Kenya Uhuru Kenyata akiwa pamoja na naibu wake William Ruto walipotangaza muungano wao wa Jubilee kabla ya uchaguzi wa mwaka wa 2013.
Rais wa Kenya Uhuru Kenyata akiwa pamoja na naibu wake William Ruto walipotangaza muungano wao wa Jubilee kabla ya uchaguzi wa mwaka wa 2013.

Vyama mbali mbali vya kisiasa nchini Kenya vilivunjwa siku ya Alhamisi Septemba 8, 2016 na kujiunga na chama kipya cha Jubilee Party katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Bomas of Kenya mjini Nairobi.

Moja kati ya vyama hivyo ni United Republican Party (URP) kilicho na takriban wabunge 70 katika bunge la taifa. Aden Duale, ambaye ni kiongozi wa shughuli za serikali bungeni na ambaye alitoa hotuba kwa niaba ya kiongozi wa chama hicho William Ruto, alizungumza na Sauti ya Amerika siku ya Alhamisi na kueleza zaidi umuhimu wa hatua hiyo.

please wait

No media source currently available

0:00 0:03:03 0:00
Kiungo cha moja kwa moja

XS
SM
MD
LG