Maafisa nchini Kenya wanasema jengo moja lililoporomoka katika mji mkuu wa Nairobi limesababisho vifo vya watu wawili na wengine kukwama ndani.
Maafisa wa usalama wanasema jengo hilo la ghorofa sita lilikuwa katika ujenzi limeporomoka leo.
Kundi la uokozi liko katika eneo la tukio kutafuta waliokwama ndani ya mabaki ya jengo hilo.
Shirika la msalaba mwekundu la Kenya limesema idadi kadhaa ya watu wamejeruhiwa baada ya jengo hilo kuporomoka ingawa halikusema ni watu wangapi.
Jengo hilo la ghorofa sita liko karibu na uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta mashariki mwa Nairobi . Chanzo cha ajali hiyo bado hakijaelezwa.