Wataalamu wa maswala ya maji kutoka takriban mataifa 40 ya bara Afrika wanakongamana jijini Nairobi kujadili upatikanaji wa maji safi na pia kuchughulikia kusafishwa kwa maji taka.
Wataalamu hao wanakutana kwa kipindi cha siku nne kuangazia maswala mbali mbali kuhusu maji na jinsi ya kushughulisha umma barani Afrika kuhifadhi vyanzo vya maji na pia kukidhi mahitaji ya maji barani humo.