Muafaka unakaribia kupatikana kati ya vyama vikuu vya kisiasa nchini Kenya kuhusiana na mikakati ya kuvunjwa na kubuniwa upya kwa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka, IEBC kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka ujao.
Vyama vya upinzani vimefutilia mbali maandamano ambayo yamekuwa yakishuhudiwa nchini humo katika siku za hivi karibuni kutokana na swala hilo.Siku ya Jumatano, mabunge yote mawili yanatarajiwa kujadili hoja kutoka kwa kamati ya shughuli japo kutoaminiana kunaendelea kushudiwa kila wakati viongozi wanapotoa hotuba kwa wafuasi wao.
Kwa taarifa zaidi sikiliza ripoti ya Josephat Kioko, mwandishi wa VOA kutoka Mombasa .