Idara ya Ulinzi ya Kenya imesema haiwezi kutangaza hadharani idadi ya wanajeshi waliouawa nchini Somalia mapema Ijumaa iliopita,kabla ya kufahamisha familia zao.
Wakati huo huo mamlaka ya inaendelea kufuatilia kwa makini watu wanaodaiwa kusambaza picha kupitia mitandao ya kijamii,zinzazoonyesha wanajeshi wengi wakiwa wameuwawa na wanamgambo wa Al Shabaab.
Mkuu wa jeshi la Kenya la KDF, Samson Mwathethe amesema kuwa shambulizi hilo lilisababisha maafa wa wanajeshi wa muungano na vile vile wanamgambo wa Al shabab.