Mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC inasema imewahurusu waendesha mashitaka kuanza uchunguzi katika uwezekano wa kuwepo kwa uhalifu wa kivita huko Ivory Coast.
Mahakama yenye makao makuu yake The Hague ilisema katika taarifa Jumatatu inaruhusu ombi la mwendesha mashitaka Luis Moreno-Ocampo kutaka uchunguzi ufanyike kuhusu ghasia za baada ya uchaguzi katika taifa hilo la Afrika Magharibi kuanzia Novemba 2010.
Moreno Ocampo aliomba kupewa idhini hiyo mwezi Juni , akisema watu wapatao 3000 waliuwawa katika miezi mitano ya mapigano ya kupigania madaraka kufuatia kuchaguliwa kwa rais Alassane Outtara. Vile vile alisema zaidi ya watu 500 walikamatwa na kushikiliwa kiholela na wengine wapatao 100 waliripotiwa kubakwa.
ICC ilieleza Jumatatu kwamba imemuomba mwendesha mashtaka kuwasilisha katika kipindi cha mwezi mmoja habari juu uhalifu wowote mwengine muhimu ambao huenda ulitendeka kati ya 2002 na 2010.