Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 20, 2024 Local time: 02:20

Hong Kong yaadhimisha kupata kwa mamlaka yake


Maelfu ya watu wamefurika katika barabara za Hong Kong leo Ijumaa, wakati mji huo ukiadhimisha miaka kumi na tisa tangu kukabidhiwa kwa China kutoka kwa udhibiti wa Uingereza.

Lakini huku maafisa wa Serikali na wananchi wakihudhuria hafla ya kuipandisha bendera katika bustani ya Golden Bauhinia leo asubuhi, umati mkubwa zaidi wa watu ulikusanyika na kufanya maandamano ya kupinga kutawaliwa na China, na pia kumpinga kiongozi mwandmizi wa Hong Kong, Leung Chun-Ying, ambaye wanasema kwamba andhibitiwa na Beijing.

XS
SM
MD
LG