Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 08:43

Mtoto wa afisa wa Kenya alikuwa mmoja wa washambuliaji


Polisi akifanya doria mbele ya kanisa katoliki Garissa Jumapili, April 5, 2015.
Polisi akifanya doria mbele ya kanisa katoliki Garissa Jumapili, April 5, 2015.

Maafisa wa Kenya wanasema wamemtambua mmoja wa wavamizi wa al-Shabab waliouwa watu 148 chuo kikuu cha Garissa April 2 kama mtoto wa afisa wa serikali ya Kenya.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani Mwenda Njoka amesema kuwa Abdirahim Abdullahi alikuwa mmoja wa washambuliaji waliouawa katika mashambulizi ya Garissa. Msemaji afisa huyo wa serikali alikuwa ameripoti kuwa mtoto wake hajulikani alipo.

Afisa mmoja wa Garissa aliliambia shirika la habari la Reuters kuwa serikali ilikuwa na habari kuwa Abdullahi, ambaye alikuwa mwanafunzi wa sheria katika chuo kikuu cha Nairobi, alikuwa amejiunga na kundi la kigaidi la al-Shabab baada ya kumaliza chuo 2013.

Waombolezaji wakiwa nje ya hospitali Nairobi kutafuta maiti za ndugu zao
Waombolezaji wakiwa nje ya hospitali Nairobi kutafuta maiti za ndugu zao

Wakati huo huo, makanisa nchini Kenya yalitumia walinzi wenye bunduki kulinda waumini wao Jumapili wakati misa za Pasaka zikifanywa maalum kuwaombea waliouawa na kujeruhiwa katika mashambulizi ya Alhamisi.

Kwa mamia ya wakristo Garissa misa za Jumapili zilijaa majonzi kutokana na shambulizi hilo. Watu wenye bunduki walivamia chuo kikuu cha Garissa Alhamisi April 2 na kufyatua risasi na kuuwa watu 148 wengi wao wakristo, ingawa al-Shabab inajulikana pia kwa kuuwa waislamu katika siku za nyuma.

XS
SM
MD
LG