Wagombea urais nchini Uganda wametoa ujumbe wao wa mwisho kwa wapiga kura, saa chache baada ya mda wa mwisho wa kampeni kumalizika.
Rais Yoweri Museveni amesema hana ushindani katika uchaguzi wa Alhamisi huku naye kigogo wa upinzani, Dkt Kiiza Besigye akiomba msaada kutoka nchi za nje kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa njia huru na ya haki.
Amama Mbabazi kwa upande wake ameiomba Tume ya uchaguzi kuheshimu uamuzi wa wapiga kura.
.