Hali ya taharuki ilatanda mjini Bujumbura mapema Jumatatu, baada ya milipuko kusikika katika sehemu tofauti za mji na kusababisha majeraha kwa watu kadhaa.
Haikubainika mara moja kilichosababisha milipuko hiyo lakini msemaji wa idara ya polisi alitoa taarifa akisema kuwa hali ya usalama ilikuwa imerejeshwa na kwamba uchunguzi unaendelea ili kubainisha kilichosababisha.