Magavana wanne kutoka Sudan Kusini na pia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC wamekutana Alahamisi katika eneo la Ituri kaskazini mashariki mwa Congo kuzungumzia swala la usalama kwenye mpaka wa nchi hizo mbili pamoja na tatizo la wakimbizi kutoka Sudan Kusini ambao ni wengi kushinda eneo walilopewa hifadhi ndani ya Congo bila kupata misaada ya kibinadamu.
Wakati huo huo , Serikali ya Congo imesema kuwa haina habari zozote kuhusu aliko kiongozi wa uwasi na aliekuwa naibu wa kwanza wa Rais Sudan Kusini Riek Machar kama anavyoripoti mwandindishi wa VOA Austere Malivika akiwa DRC.
Bonyeza kwa taarifa zaidi.