Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 18, 2024 Local time: 20:46

Bush ahimiza kutopunguza msaada kwa vita dhidi ya ukimwi


Rais wa zamani wa Marekani George W.Bush akiwa pembeni ya mwanamke mwenye HIV kwenye kituo cha matibabu huko Addis Ababa .
Rais wa zamani wa Marekani George W.Bush akiwa pembeni ya mwanamke mwenye HIV kwenye kituo cha matibabu huko Addis Ababa .

Rais Bush asema mapambano dhidi ya Ukimwi lazima yaendelee licha ya wakati huu mgumu wa kiuchumi kwa wamarekani.

Rais wa zamani wa Marekani George W. Bush ameuambia mkutano mmoja wa kimataifa juu ya UKIMWI kwamba licha ya wasi wasi wa kimataifa , mapambano dhidi ya ugonjwa wa UKIMWI lazima yaendelee.

Katika hotuba ya ufunguzi Jumapili katika mji mkuu wa Ethiopia Addis Ababa Bw. Bush amesema dunia lazima iweke mambo ya lazima kwanza na hakuna umuhimu mkubwa kama kuokoa maisha ya watu.

Pia amehimiza Marekani kuzidi kuhimiza jitihada ya kuokoa maisha katika dunia inayoendelea na kuchangia vita dhidi ya kupambana na magonjwa ya zinaa yanayoambukiza na kusema kujitenga ni kutokuona mbali.

XS
SM
MD
LG