Wabunge nchini Uganda Jumanne wameanza kukusana saini ili kushinikiza bunge kurejea vikao vyake na kukatiza likizo, ili kujadili hali ya wasiwasi wa kisiasa kufuatia hatua ya Serikali ya kumuweka aliekuwa mgombea urais wa upinzani Dkt Kiiza Besigye chini ya ulin zi mkali wa Polisi.
Hayo yanajiri wakati Besigye akiripotiwa kukwepa mtego wa Polisi nyumbani kwake na kusafiri kupitia uwanja wa ndege akielekea Marekani kama anavyoeleza mwandishi wa VOA Kennes Bwire akiwa Kampala.
Bonyeza usikilize.