Mgombea wa urais nchini Uganda kwa tiketi ya chama cha Forum for democratic change-FDC Dkt. Kiiza Besigye, ametoa changamoto kwa mwenzake wa chama tawala cha National resistance movement-NRM rais Yoweri Museveni, kutokwepa mdahalo wa pamoja wa wagombea wote wa urais unaotarajiwa kufanyika siku ya Ijumaa wiki ijayo.
Besigye alikuwa akihutubia umati mkubwa wa watu mashariki mwa Uganda katika mji wa Mbale akiwa kwenye uwanja mmoja mjini humo uliojaa watu kupita kiasi.
Mdahalo huo umeandaliwa na taasisi za kidini na Besigye anasema itawapa wananchi wa Uganda kuchambua mbivu na mbichi kisiasa.