Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon Jumanne alitembea mashariki mwa Congo ambako alikutana na wakimbizi katika eneo la Masisi kwenye kijiji cha Kichanga kilomita 80 kaskazini magharibi mwa Mji wa Goma huko, Kivu kaskzini.
Wakimbizi hao waliomba Umoja wa Mataifa uwasasidie kupata
Amani ili warudi kwenye vijiji vyao wakisema walikuwa wamechoshwa na maisha ya ukimbizi.
Katibu huyo amewaahidi kuwa atakutana na Rais Joseph Kabila ili serikali
ya Congo ishirikiane na kikosi cha Umoja wa Mataifa, MONUSCO katika kutokomeza makundi ya waasi yalioko mashariki mwa nchii hiyo.