Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 00:29

Ban Ki Moon apendekeza walinda amani zaidi Jamhuri ya Afrika ya Kati


Mpiganaji wa kundi la wanamgambo wanaojiita "anti-balaka" akiwa na panga mdomoni Februari 22, 2014.
Mpiganaji wa kundi la wanamgambo wanaojiita "anti-balaka" akiwa na panga mdomoni Februari 22, 2014.

Siku za nyuma Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa alionya kuwa ghasia nchini humo huenda zikaleta migawanyiko.

Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki Moon amependekeza karibu kikosi cha askari 12,000 wa kulinda amani wa umoja wa Afrika kupelekwa Jamhuri ya Afrika ya Kati ambapo vurugu za kidini hazionyeshi dalili za kudhibitiwa .

Katika ripoti yake kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa Jumatatu Bw.Ban alisema jukumu la kwanza la jeshi hilo litakuwa kulinda raia.

Bw.Ban aliwahi kusema siku za nyuma kwamba ana wasiwasi ghasia hizo za Jamhuri ya Afrika ya Kati huenda zikasababisha migawanyiko nchini humo.
XS
SM
MD
LG