Kwenye uchaguzi wa Rais hapa Marekani mwaka huu, swala la nyongeza ya mishahara kwa wafanyakazi wa kipato cha chini ni muhimu mno na limezua gumzo kuhusu kurejesha nafasi za kazi kwa wananchi. Baadhi ya wamarekani kwa hakika wameelezea hofu zao kuhusu kipato na gharama ya maisha inayoendelea kupanda kila uchao.
Swala jingine nyeti katika kampeni hizo ni tofauti za mapato miongoni mwa wamarekani ambapo utafiti umebaini kuwa watu milioni 49 nchini Marekani wanaishi katika hali ya umasikini akiwemo mtoto mmoja kwa kila wanne kama wanavyosimulia waandishi wa VOA, BMJ Murrithi na Harrison Kamau .
Bonyeza usikilize.