Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 09:28

Jeshi la Rwanda limewakamata majenerali waandamizi


Jeshi la Rwanda limewakamata majenerali waandamizi
Jeshi la Rwanda limewakamata majenerali waandamizi

<!-- IMAGE -->

Jeshi la Rwanda limesema limewakamata majenerali wawili wa vyeo vya juu kwa tuhuma za rushwa na utovu wa nidhamu ikiwa ni pamoja na naibu mkuu wa zamani wa kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa katika eneo la Darfur nchini Sudan.

Jeshi limesema limemkamata naibu mkuu wa zamani Meja Jenerali Emanuel Karenzi Karake kwa tabia ambayo inakiuka misingi ya jeshi la Rwanda.

Msemaji wa Jeshi Jill Rutaremara amesema maafisa pia wamewakamata mkuu mpya wa jeshi la akiba la Rwanda Luteni Jenerali Charles Muhire.

Muhire anatuhumiwa kwa rushwa na kutumia vibaya madaraka.

XS
SM
MD
LG