Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 20, 2024 Local time: 03:56

Obama afanya ziara ya kushtukiza Afghanistan


Obama afanya ziara ya kushtukiza Afghanistan
Obama afanya ziara ya kushtukiza Afghanistan
<!-- IMAGE -->

Rais wa Marekani Barack Obama ameondoka Afghanistan mapema leo Jumatatu baada ya ziara fupi ya kushtukiza, ambapo aliisifia serikali ya Afghanistan kupambana na rushwa na kuimarisha utawala wake.

Bwana Obama alitumia muda usiozidi saa 6 nchini humo katika ziara yake ya kwanza kama Rais kuelekea Afghanistan.

Rais Obama alimwambia kiongozi mwenzake wa Afghanistan, Hamid Karzai na baraza lake la mawaziri huko Kabul Jumapili, wanahitajika kupambana na rushwa na kuongeza kanuni za sheria.

XS
SM
MD
LG