Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 25, 2024 Local time: 17:05

Ghasia za kidini zaibuka tena Nigeria


Watu 13 wameuwawa katika ghasia nyingine za kidini na kikabila zilizotokea Nigeria ya kati.

Maafisa wanasema wafugaji wa kiislam walivamia kijiji cha wakristo kusini mwa mji wa Jos mapema leo wakichoma nyumba na kushambulia watu kwa mapanga huku wakikimbia nje.

Mashahidi wanasema washambuliaji hao walivalia sare za kijeshi.

Mji wa Jos na vitongoji vyake una historia ya ghasia za kidiini ikiwa inachochewa kwa kiasi fulani na ushindani wa udhibiti wa maeneo yenye rutuba.

XS
SM
MD
LG