Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 20, 2024 Local time: 00:10

Marekani yahimiza mabadiliko ya utawala Burma


Afisa wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani amesema juhudi za marekani kwa Burma za kushawishi marekebisho ya kisiasa zimekuwa na matokeo mchanganyiko na ameonya kuwa uvumilivu wa uongozi wa rais Barack Obama hauna kiwango. Kurt Campbell waziri mdogo wa masuala ya Asia na pacific alisema jumamnne kuwa anatarajia mawasiliano zaidi na Burma. Aliwaambia waandishi wa habari kuwa yeye na waziri wa mambo ya nje Hillary Clinton wanatarajia mabadiliko ya wazi katika wiki zijazo kuhusu inakoelekea serikali ya kijeshi ya Burma.

XS
SM
MD
LG