Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 00:26

Haiti yakumbwa na mtetemeko wa Ardhi


Tetemeko la ardhi la kiwango cha 7.0, limepiga kisiwa cha Haiti, na kusababisha majengo katika mji mkuu, Port-au-Prince, kuporomoka na kuzusha hali ya wasiwasi mkubwa kisiwani humo.

Kuna taarifa kwamba makazi ya Rais na majengo mengine ya serikali huko Port-au-Prince, yameharibika vibaya, pamoja na nyumba nyingi. Ripoti za vifo na majeruhi hazijathibitishwa, kwa sababu mawasiliano katika mji mkuu na sehemu nyingine yameathiriwa vibaya, na kuna tatizo la umeme.

Wataalamu wanasema tetemeko la jana Jumanne, ni kubwa mno kuwahi kutokea kwenye eneo hilo katika muda wa miaka 200.


XS
SM
MD
LG