Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 12:52

Obama asema hatokubali kushindwa na mageuzi ya afya


Rais Obama aliliachia bunge kuandika vipengele muhimu vya mpango wake wa mageuzi ya bima ya afya, ambao hivi sasa unakabiliwa na upinzani mkali kote nchini.
Bunge hivi sasa liko katika likizo yake ya mwezi Augusti, lakini wabunge wamekuwa wakifanya mikutano katika kumbi za miji, kote nchini, ili kusikia maoni ya watu kuhusu mageuzi hayo, na wamesikia mengi, kutoka umati wa watu wanounga na wanopinga mpango huo.
Rais Obama akiwa katika mikutano yake kuteetea mapendekezo yake amewambia watu kwamba habari zinazotolewa kuhusiana na mpango wake kwa sehemu kubwa haiambatani na mpango wenyewe.
“Kila mara tunapokaribia kupitisha mswada wa mageuzi ya bima ya afya, walinda maslahi wanaturudisha nyuma na kila kitu tulicho kubaliana. Wanatumia ushawishi wao, na washirika wao wa kisiasa kututisha, na kupotosha wamarekani. Wanafanya matangazo. Hivi ndivyo wanavyofanya siku zote hatuwezi kuwaruhusu waendele kufanya hivi. Sio kwa wakati huu.”
Lakini kwa sehemu fulani upinzani, unatokana na makadirio ya gharama, kutoka idara huru, ya afisi ya hazina ya bunge la Marekani. Na kwa upande mwengine baadhi ya watu wanasema hawajapata maelezo ya kutosha kuhusu mpango huo, ili kuwawezesha kufanya uwamuzi muafaka.
Malengo mawili makuu ya mpango huo wa mageuzi, ni kupanua bima hiyo ya afya, ili kuwahudumia mamilioni ya wamarekani wasio na bima ya afya, na pili kuweza kudhibiti kupanda sana gharama za huduma kwa wale ambao tayari wenye bima ya afya.
Mpango wa bima wa uma, umependekezwa kuweza kushindana na makampuni ya binafsi ya bima. Warepublican na wapinzani wengine wanasema kwamba wazo la mageuzi la wademocrat, itapelkea kuwepo na huduma za afya za mfumo wa kijamaa au kisocialisti.

XS
SM
MD
LG