Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 16:43

Rwanda yaidhinisha uandikishaji wa chama kipya


Kigali - Serikali ya Rwanda imeidhinisha uandikishaji wa chama cha upinzani baada ya kukitalia mapema mwaka huu kwa tuhuma za kutofuata kanuni. Baraza la mawaziri la Rwanda lilikipa ridhaa ya kisheria chama cha Social Party Imberakuri katika mkutano uliofanyika alhamisi. Baraza hilo mwezi March liliyakataa maombi ya chama hicho, wakisema kimeshindwa kutekeleza vigezo kadhaa, kama vile kuteua asilimia 30 ya wanawake katika nafasi za juu za chama hicho.

XS
SM
MD
LG