Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Machi 30, 2024 Local time: 08:34

Uzalishaji mafuta wapungua Nigeria


Waziri wa Mafuta wa Nigeria anasema kiwango cha mafuta nchini humo kimeshuka kwa zaidi ya asilimia 50 kutokana na harakati za wanamgambo katika mkoa wa Niger Delta. Waziri Rilwanu Lukman anasema uzalishaji wa kila siku ni chini ya mapipa milioni mbili. Wanamgambo wamefanya wimbi la mashambulizi katika vinu vya mafuta Nigeria tangu mwanzoni mwa mwezi June, baada ya jeshi la Nigeria kuanzisha operesheni dhidi ya wanamgambo huko Niger Delta.

XS
SM
MD
LG