Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 18, 2024 Local time: 23:19

Meli Yatekwa Nyara, Kapteni Ashikiliwa Mateka


Shirika la habari la Associated Press linaripoti kuwa mfanyakazi mmoja aliyewasiliana nao kwa simu anasema kapteni wa meli hiyo bado anashikiliwa mateka ndani ya boti karibu na mali hiyo na kwamba majadiliano yanaendelea kwa lengo la kufanikisha kuachiwa kwake.

Mashirika ya habari yanawanukuu maofisa wa Marekani wakisema awali wafanyakazi wa meli walimkamata haramia mmoja, hatua ambayo imewawezesha kuachiwa kwao.

Meli hiyo 'Maersk Alabama' yenye uzito wa tani 17,000 ni mali ya Denmark na ilitekwa nyara Jumatano umali wa kilomita 450 kusini mashariki mwa Eyl, mji uliopo kaskazini mwa jimbo la Puntland nchini Somalia.

Zinazohusiana

XS
SM
MD
LG