Hali katika mji huo ilikuwa tulivu jana baada ya majeshi ya nchi hiyo kuweka amri ya kutotoka nje katika baadhi ya maeneo ya mji huo. Maofisa wa Nigeria wanasema polisi wamekamata mamia ya watu wanaodhaniwa kuhusika na mapigano hayo.
Msikiti mkubwa katika mji wa Jos unaripoti kuwa ulipokea miili ya watu wasiopungua 350 waliouwawa katika machafuko hayo, wengi wao walizikwa haraka na ndugu zao.
Haijulikani ni watu wangapi ambao siyo waislam waliuwawa katika mji wa Jos ambao ni mji mkuu wa Plateau nchini Nigeria.